Wagalatia 6 Swahili & English
Listen/Download AudioWagalatia 6 (Swahili) | Galatians 6 (English) |
---|---|
Ndugu zangu, mtu akighafilika katika kosa lo lote, ninyi mlio wa Roho mrejezeni upya mtu kama huyo kwa roho ya upole, ukijiangalia nafsi yako usije ukajaribiwa wewe mwenyewe. Wagalatia 6:1 |
Brothers, even if a man is caught in some fault, you who are spiritual must restore such a one in a spirit of gentleness; looking to yourself so that you also aren't tempted. |
Mchukuliane mizigo na kuitimiza hivyo sheria ya Kristo. Wagalatia 6:2 |
Bear one another's burdens, and so fulfill the law of Christ. |
Maana mtu akijiona kuwa ni kitu, naye si kitu, ajidanganya nafsi yake. Wagalatia 6:3 |
For if a man thinks himself to be something when he is nothing, he deceives himself. |
Lakini kila mtu na aipime kazi yake mwenyewe, ndipo atakapokuwa na sababu ya kujisifu ndani ya nafsi yake tu, wala si kwa mwenzake. Wagalatia 6:4 |
But let each man test his own work, and then he will take pride in himself and not in his neighbor. |
Maana kila mtu atalichukua furushi lake mwenyewe. Wagalatia 6:5 |
For each man will bear his own burden. |
Mwanafunzi na amshirikishe mkufunzi wake katika mema yote. Wagalatia 6:6 |
But let him who is taught in the word share all good things with him who teaches. |
Msidanganyike, Mungu hadhihakiwi; kwa kuwa cho chote apandacho mtu, ndicho atakachovuna. Wagalatia 6:7 |
Don't be deceived. God is not mocked, for whatever a man sows, that will he also reap. |
Maana yeye apandaye kwa mwili wake, katika mwili wake atavuna uharibifu; bali yeye apandaye kwa Roho, katika Roho atavuna uzima wa milele. Wagalatia 6:8 |
For he who sows to his own flesh will from the flesh reap corruption. But he who sows to the Spirit will from the Spirit reap eternal life. |
Tena tusichoke katika kutenda mema; maana tutavuna kwa wakati wake, tusipozimia roho. Wagalatia 6:9 |
Let us not be weary in doing good, for we will reap in due season, if we don't give up. |
Kwa hiyo kadiri tupatavyo nafasi na tuwatendee watu wote mema; na hasa jamaa ya waaminio. Wagalatia 6:10 |
So then, as we have opportunity, let's do what is good toward all men, and especially toward those who are of the household of the faith. |
Tazameni ni kwa herufi gani kubwa nimewaandikia kwa mkono wangu mimi mwenyewe! Wagalatia 6:11 |
See with what large letters I write to you with my own hand. |
Wote watakao kuonekana ni wazuri kwa mambo ya mwili, ndio wanaowashurutisha kutahiriwa; makusudi wasiudhiwe kwa ajili ya msalaba wa Kristo, hilo tu. Wagalatia 6:12 |
As many as desire to look good in the flesh, they compel you to be circumcised; only that they may not be persecuted for the cross of Christ. |
Kwa maana hata wao wenyewe waliotahiriwa hawaishiki sheria; bali wanataka ninyi mtahiriwe, wapate kuona fahari katika miili yenu. Wagalatia 6:13 |
For even they who receive circumcision don't keep the law themselves, but they desire to have you circumcised, that they may boast in your flesh. |
Lakini mimi, hasha, nisione fahari juu ya kitu cho chote ila msalaba wa Bwana wetu Yesu Kristo, ambao kwa huo ulimwengu umesulibishwa kwangu, na mimi kwa ulimwengu. Wagalatia 6:14 |
But far be it from me to boast, except in the cross of our Lord Jesus Christ, through which the world has been crucified to me, and I to the world. |
Kwa sababu kutahiriwa si kitu, wala kutokutahiriwa, bali kiumbe kipya. Wagalatia 6:15 |
For in Christ Jesus neither is circumcision anything, nor uncircumcision, but a new creation. |
Na wote watakaoenenda kwa kanuni hiyo, amani na iwe kwao na rehema, naam, kwa Israeli wa Mungu. Wagalatia 6:16 |
As many as walk by this rule, peace and mercy be on them, and on God's Israel. |
Tangu sasa mtu asinitaabishe; kwa maana ninachukua mwilini mwangu chapa zake Yesu. Wagalatia 6:17 |
From now on, let no one cause me any trouble, for I bear the marks of the Lord Jesus branded on my body. |
Ndugu zangu, neema ya Bwana wetu Yesu Kristo na iwe pamoja na roho zenu. Amina. Wagalatia 6:18 |
The grace of our Lord Jesus Christ be with your spirit, brothers. Amen. |