Zaburi BSB

Zaburi 38

Psalms Chapter 38

1
Ee Bwana, usinilaumu katika ghadhabu yako, Wala usiniadhibu kwa ukali wa hasira yako.
A Psalm of David, for remembrance. O LORD, do not rebuke me in Your anger or discipline me in Your wrath.
2
Kwa maana mishale yako imenichoma, Na mkono wako umenipata.
For Your arrows have pierced me deeply, and Your hand has pressed down on me.
3
Hamna uzima katika mwili wangu Kwa sababu ya ghadhabu yako. Wala hamna amani mifupani mwangu Kwa sababu ya hatia zangu.
There is no soundness in my body because of Your anger; there is no rest in my bones because of my sin.
4
Maana dhambi zangu zimenifunikiza kichwa, Kama mzigo mzito zimenilemea mno.
For my iniquities have overwhelmed me; they are a burden too heavy to bear.
5
Jeraha zangu zinanuka, zimeoza, Kwa sababu ya upumbavu wangu.
My wounds are foul and festering because of my sinful folly.
6
Nimepindika na kuinama sana, Mchana kutwa nimekwenda nikihuzunika.
I am bent and brought low; all day long I go about mourning.
7
Maana viuno vyangu vimejaa homa, Wala hamna uzima katika mwili wangu.
For my loins are full of burning pain, and no soundness remains in my body.
8
Nimedhoofika na kuchubuka sana, Nimeugua kwa fadhaa ya moyo wangu.
I am numb and badly crushed; I groan in anguish of heart.
9
Bwana, haja zangu zote ziko mbele zako, Kuugua kwangu hakukusitirika kwako.
O Lord, my every desire is before You; my groaning is not hidden from You.
10
Moyo wangu unapwita-pwita, Nguvu zangu zimeniacha; Nuru ya macho yangu nayo imeniondoka.
My heart pounds, my strength fails, and even the light of my eyes has faded.
11
Wanipendao na rafiki zangu wanasimama mbali na pigo langu; Naam, karibu zangu wamesimama mbali.
My beloved and friends shun my disease, and my kinsmen stand at a distance.
12
Nao wanaoutafuta uhai wangu hutega mitego; Nao wanaotaka kunidhuru hunena mabaya; Na kufikiri hila mchana kutwa.
Those who seek my life lay snares; those who wish me harm speak destruction, plotting deceit all day long.
13
Lakini kama kiziwi sisikii, Nami ni kama bubu asiyefumbua kinywa chake.
But like a deaf man, I do not hear; and like a mute man, I do not open my mouth.
14
Naam, nimekuwa kama mtu asiyesikia, Ambaye hamna hoja kinywani mwake.
I am like a man who cannot hear, whose mouth offers no reply.
15
Kwa kuwa nakungoja Wewe, Bwana, Wewe utajibu, Ee Bwana, Mungu wangu.
I wait for You, O LORD; You will answer, O Lord my God.
16
Maana nalisema, Wasije wakanifurahia; Mguu wangu ukiteleza wajitukuza juu yangu.
For I said, “Let them not gloat over me—those who taunt me when my foot slips.”
17
Kwa maana mimi ni karibu na kusita, Na maumivu yangu yako mbele yangu daima.
For I am ready to fall, and my pain is ever with me.
18
Kwa maana nitaungama uovu wangu, Na kusikitika kwa dhambi zangu.
Yes, I confess my iniquity; I am troubled by my sin.
19
Lakini adui zangu ni wazima wenye nguvu, Nao wanaonichukia bure wamekuwa wengi.
Many are my enemies without cause, and many hate me without reason.
20
Naam, wakilipa mabaya kwa mema, Huwa adui zangu kwa kuwa nalifuata lililo jema.
Those who repay my good with evil attack me for pursuing the good.
21
Wewe, Bwana, usiniache, Mungu wangu, usijitenge nami.
Do not forsake me, O LORD; be not far from me, O my God.
22
Ufanye haraka kunisaidia, Ee Bwana, wokovu wangu.
Come quickly to help me, O Lord my Savior.

Chagua Sura