Reuben Kigame - Enda Nasi Lyrics

Enda Nasi Lyrics

Tunaomba uwepo wako uende nasi
Ewe Bwana wa majeshi utusikie
Kama huendi nasi, hatutaki kutoka hapa
Hatuwezi pekee yetu, enda nasi
Tu watu wa shingo ngumu tusamehe
Hatufai mbele zako, turehemu
Tusafishe ee Baba, tuonyeshe uso wako
Twahitaji neema yako, enda nasi

Tutavua mapambo yetu
Na vitu vyote vya thamani kwetu
Mioyo yetu twaleta mbele zako
Tutakase na utembee nasi

Tunaomba utuonyeshe njia zako
Kwa maana umetuita kwa jina
Twalilia Ee Bwana, utukufu na uso wako
Bila wewe tutashindwa, enda nasi

Tutavua mapambo yetu
Na vitu vyote vya thamani kwetu
Mioyo yetu twaleta mbele zako
Tutakase na utembee nasi


Enda Nasi Video

Enda Nasi Lyrics -  Reuben Kigame

Reuben Kigame Songs

Related Songs