Mungu ni pendo apenda watu,
Mungu ni pendo anipenda
Sikilizeni furaha yangu,
Mungu ni pendo, anipenda
Nilipotea katika dhambi,
nikawa mtumwa wa shetani
Sikilizeni furaha yangu,
Mungu ni pendo, anipenda
Akaja Yesu kuniokoa,
yeye kanipa kuwa huru
Sikilizeni furaha yangu,
Mungu ni pendo, anipenda
Sababu hii namtumikia,
namsifu yeye siku zote.
Sikilizeni furaha yangu,
Mungu ni pendo, anipenda