Ringtone + Christina Shusho - Tenda Wema Lyrics

Tenda Wema Lyrics

Tenda wema nenda zake wee 
Usisahau Mungu anaona 
Siku kuhukumu kuwa itafika 

Mayatima umesomesha sana 
Wenye shida umesaidia wote 
Wenye njaa umewapa chakula 
Nguo zako umepeana zote 
Hakuna anayetambua yale umetenda kwote 
Sasa naona inakupa worry nakuomba wewe usijali 
Aliyekuita anaona yote, tabariki ya siku zote 

Tenda wema nenda zako wee 
Usisahau Mungu anaona 
Siku kuhukumu kuwa itafika 

Aliwaponya wagonjwwa wao ni Yesu huyo 
Akafufua wafu wao ni Yesu Huyo 
Mwisho wakamwita pepo huyo ooh 
Na tena wakamwita Belizeburi 
Wewe si wa kwanza na hutakuwa wa mwisho 
Yesu katukanwa sembuse mwanadamu 

Tenda wema nenda zako wee 
Usingoje shukurani eeh 
Usisahau Mungu anaona 
Siku kuhukumu kuwa itafika 

Tenda wema nenda zako wee 
Usisahau Mungu anaona 
Siku kuhukumu kuwa itafika 

Utawasomesha wajue kizungu wakutusi 
Utawalisha washibe wakupige 
Wewe tenda mema, wewe tenda mema tu 

Tenda wema nenda zako wee 
Usisahau Mungu anaona 
Siku kuhukumu kuwa itafika


Tenda Wema Video

Tenda Wema  Lyrics -  Ringtone

Ringtone Songs

Related Songs