Christina Shusho + Janet Otieno - Napokea kwako Lyrics

Napokea kwako Lyrics

Maisha magumu sana nimepitia
Nikajaribu kutafuta msaada sikupata
Nikaendea mwanadamu mwisho akanidharau
Kumbe msaada wa mwanadamu unatoka kwa Mungu

Nilijua yapo wenye haki ya kubarikiwa
Kumbe Baraka ni haki ya kila mmoja

Nimebadili wazo langu namwelekea Mungu
Kwake msaada wangu unapatikana

Msaada wa mwanadamu ni wa muda mfupi
Na ni zamu yangu kubarikiwa we

Wakati ni huu wa kubarikiwa
Zamu ni yangu, sasa kupokea
Nimechoshwa na shida za dunia
Napokea kwako, Baba napokea kwako,
Napokea kwako, Baba napokea kwako,
Napokea kwako, Yesu napokea kwako
Napokea kwako, Baba napokea kwako,

Nimeamua kwenda Zaidi na Zaidi
Nimejipanga hadi nione matunda yake

Yale Mungu amewekeza ndani yangu
Najua Mungu yupo kazini kunikamilisha

Akisema nimebarikiwa nimebarikiwa tu
Hata ukipinga leo mimi nimebarikiwa tu

Mlima gani kuu sana usiloung’oa
Jaribu gani kuu sana usiloliweza
Chozi gani zito kwako usilolifuta
Ombi gani kubwa sana usilolijibu

Wakati ni huu wa kubarikiwa
Zamu ni yangu, sasa kupokea
Nimechoshwa na shida za dunia
Napokea kwako, Baba napokea kwako,
Napokea kwako, Baba napokea kwako,
Napokea kwako, Yesu napokea kwako
Napokea kwako, Baba napokea kwako

Wakati ni huu wa kubarikiwa
Zamu ni yangu, sasa kupokea
Nimechoshwa na shida za dunia
Napokea kwako, Baba napokea kwako,
Napokea kwako, Baba napokea kwako,
Napokea kwako, Yesu napokea kwako
Napokea kwako, Baba napokea kwako


Napokea kwako Video

Christina Shusho Songs

Related Songs