Wafilipi 2 Swahili & English
Listen/Download AudioWafilipi 2 (Swahili) | Philippians 2 (English) |
---|---|
Basi ikiwako faraja yo yote katika Kristo, yakiwako matulizo yo yote ya mapenzi, ukiwako ushirika wo wote wa Roho, ikiwako huruma yo yote na rehema, Wafilipi 2:1 |
If there is therefore any exhortation in Christ, if any consolation of love, if any fellowship of the Spirit, if any tender mercies and compassion, |
ijalizeni furaha yangu, ili mwe na nia moja, wenye mapenzi mamoja, wenye roho moja, mkinia mamoja. Wafilipi 2:2 |
make my joy full, by being like-minded, having the same love, being of one accord, of one mind; |
Msitende neno lo lote kwa kushindana wala kwa majivuno; bali kwa unyenyekevu, kila mtu na amhesabu mwenziwe kuwa bora kuliko nafsi yake. Wafilipi 2:3 |
doing nothing through rivalry or through conceit, but in humility, each counting others better than himself; |
Kila mtu asiangalie mambo yake mwenyewe, bali kila mtu aangalie mambo ya wengine. Wafilipi 2:4 |
each of you not just looking to his own things, but each of you also to the things of others. |
Iweni na nia iyo hiyo ndani yenu ambayo ilikuwamo pia ndani ya Kristo Yesu; Wafilipi 2:5 |
Have this in your mind, which was also in Christ Jesus, |
ambaye yeye mwanzo alikuwa yuna namna ya Mungu, naye hakuona kule kuwa sawa na Mungu kuwa ni kitu cha kushikamana nacho; Wafilipi 2:6 |
who, existing in the form of God, didn't consider it robbery to be equal with God, |
bali alijifanya kuwa hana utukufu, akatwaa namna ya mtumwa, akawa ana mfano wa wanadamu; Wafilipi 2:7 |
but emptied himself, taking the form of a servant, being made in the likeness of men. |
tena, alipoonekana ana umbo kama mwanadamu, alijinyenyekeza akawa mtii hata mauti, naam, mauti ya msalaba. Wafilipi 2:8 |
And being found in human form, he humbled himself, becoming obedient to death, yes, the death of the cross. |
Kwa hiyo tena Mungu alimwadhimisha mno, akamkirimia Jina lile lipitalo kila jina; Wafilipi 2:9 |
Therefore God also highly exalted him, and gave to him the name which is above every name; |
ili kwa jina la Yesu kila goti lipigwe, la vitu vya mbinguni, na vya duniani, na vya chini ya nchi; Wafilipi 2:10 |
that at the name of Jesus every knee should bow, of those in heaven, those on earth, and those under the earth, |
na kila ulimi ukiri ya kuwa YESU KRISTO NI Bwana, kwa utukufu wa Mungu Baba. Wafilipi 2:11 |
and that every tongue should confess that Jesus Christ is Lord, to the glory of God the Father. |
Basi, wapendwa wangu, kama vile mlivyotii sikuzote, si wakati mimi nilipokuwapo tu, bali sasa zaidi sana mimi nisipokuwapo, utimizeni wokovu wenu wenyewe kwa kuogopa na kutetemeka. Wafilipi 2:12 |
So then, my beloved, even as you have always obeyed, not only in my presence, but now much more in my absence, work out your own salvation with fear and trembling. |
Kwa maana ndiye Mungu atendaye kazi ndani yenu, kutaka kwenu na kutenda kwenu, kwa kulitimiza kusudi lake jema. Wafilipi 2:13 |
For it is God who works in you both to will and to work, for his good pleasure. |
Yatendeni mambo yote pasipo manung'uniko wala mashindano, Wafilipi 2:14 |
Do all things without murmurings and disputes, |
mpate kuwa wana wa Mungu wasio na lawama, wala udanganyifu, wasio na ila kati ya kizazi chenye ukaidi, kilichopotoka; ambao kati ya hao mnaonekana kuwa kama mianga katika ulimwengu, Wafilipi 2:15 |
that you may become blameless and harmless, children of God without blemish in the midst of a crooked and perverse generation, among whom you are seen as lights in the world, |
mkishika neno la uzima; nipate sababu ya kuona fahari katika siku ya Kristo, ya kuwa sikupiga mbio bure wala sikujitaabisha bure. Wafilipi 2:16 |
holding up the word of life; that I may have something to boast in the day of Christ, that I didn't run in vain nor labor in vain. |
Naam, hata nikimiminwa juu ya dhabihu na ibada ya imani yenu, nafurahi; tena nafurahi pamoja nanyi nyote. Wafilipi 2:17 |
Yes, and if I am poured out on the sacrifice and service of your faith, I rejoice, and rejoice with you all. |
Nanyi vivyo hivyo furahini, tena furahini pamoja nami. Wafilipi 2:18 |
In the same way, you also rejoice, and rejoice with me. |
Walakini natumaini katika Bwana Yesu kumtuma Timotheo afike kwenu karibu, nifarijiwe na mimi, nikiijua hali yenu. Wafilipi 2:19 |
But I hope in the Lord Jesus to send Timothy to you soon, that I also may be cheered up when I know how you are doing. |
Maana sina mtu mwingine mwenye nia moja nami, atakayeiangalia hali yenu kweli kweli. Wafilipi 2:20 |
For I have no one else like-minded, who will truly care about you. |
Maana wote wanatafuta vyao wenyewe, sivyo vya Kristo Yesu. Wafilipi 2:21 |
For they all seek their own, not the things of Jesus Christ. |
Ila mwajua sifa yake, ya kuwa ametumika pamoja nami kwa ajili ya Injili, kama mwana na baba yake. Wafilipi 2:22 |
But you know the proof of him, that, as a child serves a father, so he served with me in furtherance of the Gospel. |
Basi, natumaini kumtuma huyo mara, hapo nitakapojua yatakayonipata. Wafilipi 2:23 |
Therefore I hope to send him at once, as soon as I see how it will go with me. |
Nami naamini katika Bwana ya kuwa nitakuja na mimi mwenyewe hivi karibu. Wafilipi 2:24 |
But I trust in the Lord that I myself also will come shortly. |
Lakini naliona imenilazimu kumtuma kwenu Epafrodito, ndugu yangu, mtenda kazi pamoja nami, askari pamoja nami; tena ni mtume wenu na mhudumu wa mahitaji yangu. Wafilipi 2:25 |
But I counted it necessary to send to you Epaphroditus, my brother, fellow worker, fellow soldier, and your apostle and minister to my need; |
Kwa kuwa alikuwa na shauku kwenu ninyi nyote, akahuzunika sana, kwa sababu mlisikia ya kwamba alikuwa hawezi. Wafilipi 2:26 |
since he longed for you all, and was very troubled, because you had heard that he was sick. |
Kwa maana alikuwa hawezi kweli kweli, karibu na kufa; lakini Mungu alimhurumia; wala si yeye peke yake, ila na mimi pia; nisiwe na huzuni juu ya huzuni. Wafilipi 2:27 |
For indeed he was sick, nearly to death, but God had mercy on him; and not on him only, but on me also, that I might not have sorrow on sorrow. |
Kwa hiyo nimefanya bidii nyingi zaidi kumtuma, ili mtakapomwona tena mpate kufurahi, nami nipunguziwe huzuni yangu. Wafilipi 2:28 |
I have sent him therefore the more diligently, that, when you see him again, you may rejoice, and that I may be the less sorrowful. |
Mpokeeni, basi, katika Bwana, kwa furaha yote, mkawahesabu watu kama huyu kuwa watu wa kuheshimiwa. Wafilipi 2:29 |
Receive him therefore in the Lord with all joy, and hold such in honor, |
Maana kwa ajili ya kazi ya Kristo alikaribia kufa akaponza roho yake; ili kusudi ayatimize yaliyopungua katika huduma yenu kwangu. Wafilipi 2:30 |
because for the work of Christ he came near to death, risking his life to supply that which was lacking in your service toward me. |