Mwanzo 24 Swahili & English

Listen/Download Audio
Mwanzo 24 (Swahili) Genesis 24 (English)

Basi Ibrahimu alikuwa mzee mwenye miaka mingi, na Bwana alikuwa amembariki Ibrahimu katika vitu vyote. Mwanzo 24:1

Abraham was old, and well stricken in age. Yahweh had blessed Abraham in all things.

Ibrahimu akamwambia mtumishi wake, mzee wa nyumba yake, aliyetawala vitu vyake vyote, Tafadhali uutie mkono wako chini ya paja langu, Mwanzo 24:2

Abraham said to his servant, the elder of his house, who ruled over all that he had, "Please put your hand under my thigh.

nami nitakuapisha kwa Bwana, Mungu wa mbingu, na Mungu wa nchi, kwamba hutamtwalia mwanangu mke katika binti za Wakanaani ambao nakaa kati yao; Mwanzo 24:3

I will make you swear by Yahweh, the God of heaven and the God of the earth, that you shall not take a wife for my son of the daughters of the Canaanites, among whom I live.

bali enenda hata nchi yangu, na kwa jamaa zangu, ukamtwalie mwanangu Isaka mke. Mwanzo 24:4

But you shall go to my country, and to my relatives, and take a wife for my son Isaac."

Yule mtumishi akamwambia, Labda yule mwanamke hatakubali kufuatana nami mpaka nchi hii, je! Nimrudishe mwanao mpaka nchi ulikotoka? Mwanzo 24:5

The servant said to him, "What if the woman isn't willing to follow me to this land? Must I bring your son again to the land you came from?"

Ibrahimu akamwambia, Ujihadhari, usimrudishe mwanangu huko. Mwanzo 24:6

Abraham said to him, "Beware that you don't bring my son there again.

Bwana, Mungu wa mbingu, aliyenitoa katika nyumba ya babangu, na kusema nami katika nchi niliyozaliwa, aliniapia akisema, Nitawapa uzao wako nchi hii; yeye atampeleka malaika wake mbele yako, nawe utamtwalia mwanangu mke tokea huko; Mwanzo 24:7

Yahweh, the God of heaven, who took me from my father's house, and from the land of my birth, who spoke to me, and who swore to me, saying, 'I will give this land to your seed{or, offspring}.' He will send his angel before you, and you shall take a wife for my son from there.

na yule mwanamke asipokubali kufuatana nawe, basi, utafunguliwa kiapo changu hiki; lakini usimrudishe mwanangu huko. Mwanzo 24:8

If the woman isn't willing to follow you, then you shall be clear from this my oath. Only you shall not bring my son there again."

Yule mtumishi akaweka mkono wake chini ya paja la Ibrahimu bwana wake, akamwapia katika neno hilo. Mwanzo 24:9

The servant put his hand under the thigh of Abraham his master, and swore to him concerning this matter.

Kisha huyo mtumishi akatwaa ngamia kumi katika ngamia za bwana wake akaenda zake, maana mali zote za bwana wake zilikuwa mkononi mwake, akaondoka, akaja mpaka Mesopotamia, mpaka mji wa Nahori. Mwanzo 24:10

The servant took ten camels, of his master's camels, and departed, having all goodly things of his master's in his hand. He arose, and went to Mesopotamia, to the city of Nahor.

Akawapigisha magoti ngamia nje ya mji karibu na kisima cha maji wakati wa jioni, wakati ambapo wanawake wanakwenda kuteka maji. Mwanzo 24:11

He made the camels kneel down outside the city by the well of water at the time of evening, the time that women go out to draw water.

Naye akasema, Ee Bwana, Mungu wa bwana wangu Ibrahimu, nakuomba mambo yangu uyajalie yawe heri leo, ukamfadhili bwana wangu Ibrahimu. Mwanzo 24:12

He said, "Yahweh, the God of my master Abraham, please give me success this day, and show kindness to my master Abraham.

Tazama! Nimesimama karibu na kisima cha maji, na binti za watu wa mjini wanatoka kuteka maji, Mwanzo 24:13

Behold, I am standing by the spring of water. The daughters of the men of the city are coming out to draw water.

basi na iwe hivi; yule msichana nitakayemwambia, Tua mtungi wako, nakuomba, ninywe; naye akasema, Unywe, nami nitawanywesha na ngamia zako pia; basi huyu na awe ndiye uliyemchagulia mtumishi wako Isaka; na kwa hayo nitajua ya kuwa umemfadhili bwana wangu. Mwanzo 24:14

Let it happen, that the young lady to whom I will say, 'Please let down your pitcher, that I may drink.' She will say, 'Drink, and I will also give your camels a drink.' Let the same be she who you have appointed for your servant Isaac. Thereby will I know that you have shown kindness to my master."

Ikawa, kabla hajaisha kunena, tazama, Rebeka anatokea, binti wa Bethueli mwana wa Milka, mkewe Nahori, ndugu wa Ibrahimu, naye ana mtungi begani pake. Mwanzo 24:15

It happened, before he had done speaking, that behold, Rebekah came out, who was born to Bethuel the son of Milcah, the wife of Nahor, Abraham's brother, with her pitcher on her shoulder.

Naye yule msichana alikuwa mzuri sana uso wake, bikira, wala mwanamume hajamjua bado; akashuka kisimani, akajaza mtungi wake, akapanda. Mwanzo 24:16

The young lady was very beautiful to look at, a virgin, neither had any man known her. She went down to the spring, filled her pitcher, and came up.

Ndipo yule mtumishi akapiga mbio kwenda kumlaki, akasema, Tafadhali unipe maji kidogo katika mtungi wako ninywe. Mwanzo 24:17

The servant ran to meet her, and said, "Please give me a drink, a little water from your pitcher."

Naye akasema, Unywe, bwana wangu, akafanya haraka, akatua mtungi wake mkononi mwake, akamnywesha. Mwanzo 24:18

She said, "Drink, my lord." She hurried, and let down her pitcher on her hand, and gave him drink.

Hata alipokwisha kumnywesha akasema, Na ngamia zako nitawatekea, hata watakapokwisha kunywa. Mwanzo 24:19

When she had done giving him drink, she said, "I will also draw for your camels, until they have done drinking."

Akafanya haraka, akamwaga maji ya mtungi wake katika birika, akapiga mbio kisimani ateke, akawatekea ngamia zake wote. Mwanzo 24:20

She hurried, and emptied her pitcher into the trough, and ran again to the well to draw, and drew for all his camels.

Basi yule mtu akamkazia macho, akanyamaza, ili ajue kwamba Bwana ameifanikisha safari yake ama sivyo. Mwanzo 24:21

The man looked steadfastly at her, holding his peace, to know whether Yahweh had made his journey prosperous or not.

Ikawa, ngamia walipokwisha kunywa, yule mtu akatwaa pete ya dhahabu, uzani wake ulikuwa nusu shekeli, na vikuku viwili kwa mikono yake, uzani wake ulikuwa shekeli kumi za dhahabu, Mwanzo 24:22

It happened, as the camels had done drinking, that the man took a golden ring of half a shekel weight, and two bracelets for her hands of ten shekels weight of gold,

akasema, U binti wa nani wewe? Tafadhali uniambie. Je! Iko nafasi katika nyumba ya baba yako tupate mahali pa kukaa kwa muda? Mwanzo 24:23

and said, "Whose daughter are you? Please tell me. Is there room in your father's house for us to lodge in?"

Akasema, Mimi ni binti wa Bethueli mwana wa Milka, aliyemzalia Nahori. Mwanzo 24:24

She said to him, "I am the daughter of Bethuel the son of Milcah, whom she bore to Nahor."

Tena akamwambia, Kwetu kuna majani na malisho ya kutosha, na mahali pa kukaa wageni. Mwanzo 24:25

She said moreover to him, "We have both straw and provender enough, and room to lodge in."

Yule mtu akainama akamsujudu Bwana. Mwanzo 24:26

The man bowed his head, and worshiped Yahweh.

Akasema, Na atukuzwe Bwana, Mungu wa bwana wangu Ibrahimu, ambaye hakuacha rehema zake na kweli yake kwa bwana wangu. Bwana akaniongoza mimi nami njiani hata nyumba ya nduguze bwana wangu. Mwanzo 24:27

He said, "Blessed be Yahweh, the God of my master Abraham, who has not forsaken his loving kindness and his truth toward my master. As for me, Yahweh has led me in the way to the house of my master's relatives."

Basi yule msichana akapiga mbio, akawaambia watu wa nyumba ya mama yake mambo hayo. Mwanzo 24:28

The young lady ran, and told her mother's house about these words.

Na Rebeka alikuwa na kaka, jina lake Labani. Labani akatoka mbio kumwendea yule mtu kisimani. Mwanzo 24:29

Rebekah had a brother, and his name was Laban. Laban ran out to the man, to the spring.

Ikawa, alipoiona ile pete, na vikuku mikononi mwa nduguye, akasikia maneno ya Rebeka nduguye, akisema, Hivyo ndivyo alivyoniambia mtu huyo, basi akamjia mtu yule, na tazama, amesimama karibu na ngamia kisimani. Mwanzo 24:30

It happened, when he saw the ring, and the bracelets on his sister's hands, and when he heard the words of Rebekah his sister, saying, "This is what the man said to me," that he came to the man. Behold, he was standing by the camels at the spring.

Akasema, Karibu, wewe uliyebarikiwa na Bwana, mbona unasimama nje? Kwa maana nimeiweka nyumba tayari, na nafasi kwa ngamia. Mwanzo 24:31

He said, "Come in, you blessed of Yahweh. Why do you stand outside? For I have prepared the house, and room for the camels."

Na mtu yule akaingia katika nyumba, akawafungua ngamia; naye akatoa majani na malisho kwa ngamia, na maji ya kuoshea miguu yake, na miguu ya watu waliokuwa pamoja naye. Mwanzo 24:32

The man came into the house, and he unloaded the camels. He gave straw and provender for the camels, and water to wash his feet and the feet of the men who were with him.

Akaandaliwa chakula, lakini akasema, Sili mpaka niseme kwanza maneno yangu. Akamwambia, Haya, sema. Mwanzo 24:33

Food was set before him to eat. But he said, "I will not eat until I have told my message." He said, "Speak on."

Akasema, Mimi ni mtumwa wa Ibrahimu, Mwanzo 24:34

He said, "I am Abraham's servant.

na Bwana amembarikia sana bwana wangu, amekuwa mtu mkuu; amempa kondoo, na ng'ombe, na fedha, na dhahabu, na watumwa, na wajakazi, na ngamia, na punda. Mwanzo 24:35

Yahweh has blessed my master greatly. He has become great. He has given him flocks and herds, silver and gold, men-servants and maid-servants, and camels and donkeys.

Naye Sara, mkewe bwana wangu, akamzalia bwana wangu mwana wa kiume, katika uzee wake; naye amempa yote aliyo nayo. Mwanzo 24:36

Sarah, my master's wife, bore a son to my master when she was old. He has given all that he has to him.

Kisha bwana wangu akaniapisha akisema, Usimtwalie mwanangu mke wa binti za Wakanaani, ambao nakaa katika nchi yao. Mwanzo 24:37

My master made me swear, saying, 'You shall not take a wife for my son of the daughters of the Canaanites, in whose land I live,

Ila uende mpaka nyumbani kwa babangu, na kwa jamaa zangu, ukamtwalie mwanangu mke. Mwanzo 24:38

but you shall go to my father's house, and to my relatives, and take a wife for my son.'

Nikamwambia bwana wangu, Labda huyo mwanamke hatafuatana nami. Mwanzo 24:39

I said to my master, 'What if the woman will not follow me?'

Akaniambia, Bwana, ambaye naenenda machoni pake, atapeleka malaika wake pamoja nawe, atafanikisha njia yako; nawe umtwalie mwanangu mke katika jamaa zangu, na wa nyumba ya babangu. Mwanzo 24:40

He said to me, 'Yahweh, before whom I walk, will send his angel with you, and prosper your way. You shall take a wife for my son of my relatives, and of my father's house.

Ndipo utafunguliwa kiapo changu hapo utakapowafikilia jamaa zangu; nao wasipokupa msichana huyo, utafunguliwa kiapo changu. Mwanzo 24:41

Then will you be clear from my oath, when you come to my relatives. If they don't give her to you, you shall be clear from my oath.'

Nami nikaja leo kisimani, nikasema, Ee Bwana, Mungu wa bwana wangu Ibrahimu, ukinifanikishia sasa njia yangu niendayo mimi, Mwanzo 24:42

I came this day to the spring, and said, 'Yahweh, the God of my master Abraham, if now you do prosper my way which I go.

tazama! Nimesimama karibu na kisima cha maji; basi na iwe hivi, msichana ajaye kuteka maji, nikamwambia, Nipe, nakuomba, maji kidogo katika mtungi wako ninywe, Mwanzo 24:43

Behold, I am standing by the spring of water. Let it happen, that the maiden who comes forth to draw, to whom I will say, Give me, I pray you, a little water from your pitcher to drink.

naye akaniambia, Unywe wewe, na ngamia zako pia nitawatekea, huyo na awe ndiye mke Bwana aliyemwekea mwana wa bwana wangu. Mwanzo 24:44

She will tell me, "Drink, and I will also draw for your camels." Let the same be the woman whom Yahweh has appointed for my master's son.'

Hata kabla sijaisha kusema moyoni mwangu, tazama! Rebeka akatokea, na mtungi begani mwake. Akashuka kisimani akateka. Nami nikamwambia, Tafadhali nipe maji ninywe. Mwanzo 24:45

Before I had done speaking in my heart, behold, Rebekah came forth with her pitcher on her shoulder. She went down to the spring, and drew. I said to her, 'Please let me drink.'

Akafanya haraka akatua mtungi wake chini, akanena, Unywe, na ngamia zako nitawanywesha pia; basi nikanywa, akawanywesha na ngamia nao. Mwanzo 24:46

She hurried and let down her pitcher from her shoulder, and said, 'Drink, and I will also give your camels a drink.' So I drank, and she made the camels drink also.

Kisha nikamwuliza nikasema, U binti wa nani wewe? Naye akasema, Mimi ni binti Bethueli, mwana wa Nahori, Milka aliyemzalia. Nami nikamtia hazama puani mwake na vikuku mikononi mwake. Mwanzo 24:47

I asked her, and said, 'Whose daughter are you?' She said, 'The daughter of Bethuel, Nahor's son, whom Milcah bare to him.' I put the ring on her nose, and the bracelets on her hands.

Nikainama, nikamsujudia Bwana, nikamtukuza Bwana, Mungu wa bwana wangu Ibrahimu, aliyeniongoza njiani, nimtwalie mwana wa bwana wangu binti wa ndugu yake. Mwanzo 24:48

I bowed my head, and worshiped Yahweh, and blessed Yahweh, the God of my master Abraham, who had led me in the right way to take my master's brother's daughter for his son.

Basi, kama mnataka kumfanyia rehema na kweli bwana wangu, niambieni kama sivyo, niambieni; ili nigeuke upande wa kuume au wa kushoto. Mwanzo 24:49

Now if you will deal kindly and truly with my master, tell me. If not, tell me. That I may turn to the right hand, or to the left."

Ndipo Labani na Bethueli wakajibu wakasema, Neno hili limetoka kwa Bwana, wala sisi hatuwezi kukuambia neno jema wala baya. Mwanzo 24:50

Then Laban and Bethuel answered, "The thing proceeds from Yahweh. We can't speak to you bad or good.

Tazama, huyo Rebeka yuko mbele yako, umchukue, ukaende zako awe mke wa mwana wa bwana wako, kama alivyosema Bwana. Mwanzo 24:51

Behold, Rebekah is before you, take her, and go, and let her be your master's son's wife, as Yahweh has spoken."

Ikawa mtumishi wa Ibrahimu aliposikia maneno yao, akainama hata nchi mbele za Bwana. Mwanzo 24:52

It happened that when Abraham's servant heard their words, he bowed himself down to the earth to Yahweh.

Kisha huyo mtumishi akatoa vyombo vya fedha, na vyombo vya dhahabu, na mavazi, akampa Rebeka; na vitu vya thamani akampa nduguye na mamaye pia. Mwanzo 24:53

The servant brought forth jewels of silver, and jewels of gold, and clothing, and gave them to Rebekah. He gave also to her brother and to her mother precious things.

Wakala wakanywa, yeye na watu waliokuwa pamoja naye, nao wakakaa usiku. Wakaondoka asubuhi, naye akasema, Nipeni ruhusa niende kwa bwana wangu. Mwanzo 24:54

They ate and drank, he and the men who were with him, and stayed all night. They rose up in the morning, and he said, "Send me away to my master."

Ndugu yake na mama yake wakasema, Msichana na akae kwetu kama siku kumi, zisipungue, baadaye aende. Mwanzo 24:55

Her brother and her mother said, "Let the young lady stay with us a few days, at least ten. After that she will go."

Naye akawaambia, Msinikawilishe, mradi Bwana amefanikisha njia yangu; nipeni ruhusa niende kwa bwana wangu. Mwanzo 24:56

He said to them, "Don't hinder me, seeing Yahweh has prospered my way. Send me away that I may go to my master."

Wakasema, Na tumwite huyo msichana, tumwulize mwenyewe. Mwanzo 24:57

They said, "We will call the young lady, and ask her."

Wakamwita Rebeka wakamwuliza, Je! Utakwenda na mtu huyu? Akasema, Nitakwenda. Mwanzo 24:58

They called Rebekah, and said to her, "Will you go with this man?" She said, "I will go."

Ndipo wakampeleka Rebeka ndugu yao, na yaya wake, na mtumishi wa Ibrahimu, na watu wake. Mwanzo 24:59

They sent away Rebekah, their sister, with her nurse, Abraham's servant, and his men.

Wakambarikia Rebeka, wakamwambia, Ndugu yetu, uwe wewe mama wa kumi elfu, mara elfu nyingi, na wazao wako waurithi mlango wa hao wawachukiao. Mwanzo 24:60

They blessed Rebekah, and said to her, "Our sister, may you be the mother of thousands of ten thousands, and let your seed possess the gate of those who hate them."

Rebeka akaondoka na vijakazi wake, nao wakapanda juu ya ngamia, wakamfuata yule mtu. Naye huyo mtumishi akamchukua Rebeka akaenda zake. Mwanzo 24:61

Rebekah arose with her ladies. They rode on the camels, and followed the man. The servant took Rebekah, and went his way.

Basi Isaka alikuwa amekuja kwa njia ya Beer-lahai-roi, maana alikaa katika nchi ya kusini. Mwanzo 24:62

Isaac came from the way of Beer Lahai Roi. For he lived in the land of the South.

Isaka akatoka ili kutafakari kondeni wakati wa jioni; akainua macho yake, akaona, kuna ngamia wanakuja. Mwanzo 24:63

Isaac went out to meditate in the field at the evening. He lifted up his eyes, and saw, and, behold, there were camels coming.

Rebeka akainua macho, naye alipomwona Isaka, alishuka juu ya ngamia. Mwanzo 24:64

Rebekah lifted up her eyes, and when she saw Isaac, she dismounted from the camel.

Akamwambia mtumishi, Ni nani mtu huyu ajaye kondeni kutulaki? Mtumishi akasema, Huyu ndiye bwana wangu. Basi akatwaa shela yake akajifunika. Mwanzo 24:65

She said to the servant, "Who is the man who is walking in the field to meet us?" The servant said, "It is my master." She took her veil, and covered herself.

Yule mtumishi akamwambia Isaka mambo yote aliyoyatenda. Mwanzo 24:66

The servant told Isaac all the things that he had done.

Isaka akamwingiza Rebeka katika hema ya mama yake, Sara, akamtwaa Rebeka, akawa mkewe, akampenda; Isaka akafarijika kwa ajili ya kufa kwa mamake. Mwanzo 24:67

Isaac brought her into his mother Sarah's tent, and took Rebekah, and she became his wife. He loved her. Isaac was comforted after his mother's death.