2 Mambo ya Nyakati 17 Swahili & English
Listen/Download Audio2 Mambo ya Nyakati 17 (Swahili) | 2nd Chronicles 17 (English) |
---|---|
Na Yehoshafati mwanawe akatawala mahali pake, akajitia nguvu juu ya Israeli. 2 Mambo ya Nyakati 17:1 |
Jehoshaphat his son reigned in his place, and strengthened himself against Israel. |
Akaweka jeshi katika miji yote yenye maboma ya Yuda, akatia na askari walinzi katika nchi ya Yuda, na katika miji ya Efraimu, aliyoitwaa Asa babaye. 2 Mambo ya Nyakati 17:2 |
He placed forces in all the fortified cities of Judah, and set garrisons in the land of Judah, and in the cities of Ephraim, which Asa his father had taken. |
Naye Bwana alikuwa pamoja na Yehoshafati, kwa kuwa alikwenda katika njia za kwanza za Daudi babaye, asiyatafute mabaali; 2 Mambo ya Nyakati 17:3 |
Yahweh was with Jehoshaphat, because he walked in the first ways of his father David, and didn't seek the Baals, |
lakini alimtafuta Mungu wa baba yake, akaenda katika amri zake, wala si katika matendo ya Israeli. 2 Mambo ya Nyakati 17:4 |
but sought to the God of his father, and walked in his commandments, and not after the doings of Israel. |
Kwa hiyo Bwana akauthibitisha ufalme mkononi mwake; Yehoshafati akaletewa zawadi na Yuda wote; basi akawa na mali na heshima tele. 2 Mambo ya Nyakati 17:5 |
Therefore Yahweh established the kingdom in his hand; and all Judah brought to Jehoshaphat tribute; and he had riches and honor in abundance. |
Ukainuliwa moyo wake katika njia za Bwana; na zaidi ya hayo akapaondoa mahali pa juu, na maashera, katika Yuda. 2 Mambo ya Nyakati 17:6 |
His heart was lifted up in the ways of Yahweh: and furthermore he took away the high places and the Asherim out of Judah. |
Tena, katika mwaka wa tatu wa kutawala kwake, akawatuma wakuu wake, yaani, Ben-haili, na Obadia, na Zekaria, na Nethaneli, na Mikaya, ili kufundisha mijini mwa Yuda; 2 Mambo ya Nyakati 17:7 |
Also in the third year of his reign he sent his princes, even Ben Hail, and Obadiah, and Zechariah, and Nethanel, and Micaiah, to teach in the cities of Judah; |
na pamoja nao Walawi, yaani, Shemaya, na Nethania, na Zebadia, na Asaheli, na Shemiramothi, na Yehonathani, na Adonia, na Tobia, na Tob-adonia, Walawi; na pamoja nao Elishama na Yehoramu, makuhani. 2 Mambo ya Nyakati 17:8 |
and with them the Levites, even Shemaiah, and Nethaniah, and Zebadiah, and Asahel, and Shemiramoth, and Jehonathan, and Adonijah, and Tobijah, and Tob-adonijah, the Levites; and with them Elishama and Jehoram, the priests. |
Wakafundisha katika Yuda, wenye kitabu cha torati ya Bwana; wakazunguka katika miji yote ya Yuda, wakafundisha kati ya watu. 2 Mambo ya Nyakati 17:9 |
They taught in Judah, having the book of the law of Yahweh with them; and they went about throughout all the cities of Judah, and taught among the people. |
Hofu ya Bwana ikaziangukia falme za nchi zote zilizozunguka Yuda, wasipigane vita na Yehoshafati. 2 Mambo ya Nyakati 17:10 |
The fear of Yahweh fell on all the kingdoms of the lands that were round about Judah, so that they made no war against Jehoshaphat. |
Na baadhi ya Wafilisti walimletea Yehoshafati zawadi, na fedha ya kodi; Waarabu nao wakamletea makundi, kondoo waume saba elfu na mia saba, na mabeberu saba elfu na mia saba. 2 Mambo ya Nyakati 17:11 |
Some of the Philistines brought Jehoshaphat presents, and silver for tribute; the Arabians also brought him flocks, seven thousand and seven hundred rams, and seven thousand and seven hundred male goats. |
Ukuu wake Yehoshafati ukazidi sana; akajenga katika Yuda ngome na miji ya hazina. 2 Mambo ya Nyakati 17:12 |
Jehoshaphat grew great exceedingly; and he built in Judah castles and cities of store. |
Naye alikuwa na kazi nyingi katika miji ya Yuda; na watu wa vita, watu mashujaa humo Yerusalemu. 2 Mambo ya Nyakati 17:13 |
He had many works in the cities of Judah; and men of war, mighty men of valor, in Jerusalem. |
Na hivi ndivyo walivyohesabiwa kwa mbari za baba zao; wa Yuda, maakida wa maelfu; Adna jemadari, na pamoja naye watu mashujaa mia tatu elfu; 2 Mambo ya Nyakati 17:14 |
This was the numbering of them according to their fathers' houses: Of Judah, the captains of thousands: Adnah the captain, and with him mighty men of valor three hundred thousand; |
na wa pili wake Yehohanani akida, na pamoja naye mia mbili na themanini elfu; 2 Mambo ya Nyakati 17:15 |
and next to him Jehohanan the captain, and with him two hundred eighty thousand; |
na baada yake Amasia mwana wa Zikri, aliyejitoa kwa Bwana kwa moyo, na pamoja naye mia mbili elfu, watu mashujaa; 2 Mambo ya Nyakati 17:16 |
and next to him Amasiah the son of Zichri, who willingly offered himself to Yahweh; and with him two hundred thousand mighty men of valor. |
na wa Benyamini; Eliada mtu shujaa, na pamoja naye mia mbili elfu wenye nyuta na ngao; 2 Mambo ya Nyakati 17:17 |
Of Benjamin: Eliada a mighty man of valor, and with him two hundred thousand armed with bow and shield; |
na wa pili wake Yehozabadi, na pamoja naye mia na themanini elfu waliojiweka tayari kwa vita. 2 Mambo ya Nyakati 17:18 |
and next to him Jehozabad and with him one hundred eighty thousand ready prepared for war. |
Hao ndio waliomngojea mfalme, zaidi ya hao mfalme aliowaweka katika miji yenye maboma katika Yuda yote. 2 Mambo ya Nyakati 17:19 |
These were those who waited on the king, besides those whom the king put in the fortified cities throughout all Judah. |